Tuesday, 7 June 2016

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI Mh. WILIAM V. LUKUVI AKIWA KATIKA ZIARA WILAYANI KITETO MKOANI MANYARA LEO TAREHE 07.06.2016

Mh. W. LUKUVI ALIFUNGUA JENGO LA BALAZA LA ARDHI WILAYA KISHA ALIPATA FURSA YA KUZUNGUMZA NA WANANCHI KATIKA MKUTANO WA HADHARA ULIOFANYIKA ENEO LA VIWANJA VYA CHINI YA MTI MJINI KIBAYA.

PICHA ZA MATUKIO HAYA NI HIZI ZIFUATAZO:-

 


Hili ni jengo la Baraza la Ardhi Wilaya lilipo katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara. Jengo hili limezinduliwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. Wiliam Lukuvi leo tarehe 07.06.2016.


Mh. Lukuvi akiwahutubia wananchi katika Viwanja vya chini ya mti katikati ya Mji wa Kibaya Wilayani Kiteto



Hii ni meza kuu, kwa majina kuanzia kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri
 ya Wilaya ya Kiteto Mh. Lailumbe, anayefuata ni Mkuu wa Wilaya ya Kiteto
 Mh. Col. S. Nzoka, kisha Waziri Mh. Wiliam Lukuvi, 
Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mh. Joel Bendera na wamwisho ni 
Mbunge wa Jimbo la Kiteto Mh. E. Papian



Mh. Waziri akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mh. Joel Bendera  




Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mh. Joel Bendera akisalimiana na Mzee maarufu wa Wilaya ya Kiteto.




Upande wa kulia wanaoonekana ni Wataalamu mbalimbali

 waliohudhuria katika mkutano huo 





Wananchi wa Wilaya ya Kiteto wakimsikiliza Mh. Lukuvi akiwahutubia.




Viongozi wa Serikali kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto na Mkoa wa Manyara kwa ujumla wao wakiwa wamejumuika na wananchi katika viwanja hivyo wakimsikiliza Mh. Lukuvi akiwahutubia.


Vyombo vya ulinzi na usalama havikuwa mbali katika kuhakikisha uwepo wa usalama wa raia katika mkutano huu, kama wanavyoonekana katika gari hapo juu.

Kisha Wananchi mbalimbali walipata fursa ya kuuliza maswali kwa Serikali kama inavyoonekana picha za hapo chini.











Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bw. Bosco O. Ndunguru (wa upande wa kushoto) akitoa ufafanuzi wa baadhi ya vipengele vilivyohusu Ardhi.




Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bw. Bosco O. Ndunguru (aliyesimama mbele katikati) akiendelea na kutoa ufafanuzi wa baadhi ya vipengele vilivyohusu Ardhi.





Kaimu Mhandisi wa Ujenzi wa Wilaya ya Kiteto Bw. S. Kasturi  (aliyesimama wa kwanza kushoto ) akitoa ufafanuzi katika vipengele vilivyohusu Ujenzi.




Kaimu Afisa Ardhi  wa Wilaya ya Kiteto Bw. Guricha  akitoa ufafanuzi katika vipengele vilivyohusu Ardhi.



No comments:

Post a Comment